Thursday 10 November 2016

TRUMP Rais Mpya wa Marekani


Jana, Novemba 9, 2016, Bilionea Donald Trump wa chama cha Republican alifanikiwa kushinda uchaguzi na kuwa Rais wa 45 wa taifa kubwa duniani la Marekani, akimshinda Hillary Clinton kwa kura za wajumbe (Electoral Votes) 276 kwa 218.

Donald Trump, kwa mujibu wa Katiba ya Marekani anatarajiwa kuapishwa rasmi Januari 20, 2017 na kumrithi Baraka Obama wa Chama cha Democrat.